1. Jumapili ijayo itakuwa ni Dominika ya kumi na saba ya kipindi cha kawaida, mwaka A. Tunawashukuru wote waliofanya huduma wiki hii. Wiki ijayo huduma zitakuwa Kama ifuatavyo:
· Misa ya kwanza: saa 12:30 asub. –Neo Katekumenato
· Misa ya Pili: saa 2:00 asubuhi. – Watumishi· Misa ya Nne: saa 5:30 asub– C.M.A
· Misa ya Tatu: saa 3:30 asubuhi. –Mt. Monica Misa ya Tano: saa 11: 30 jioni
2. Siku za watakatifu juma hili:
· Jumatano, tarehe 22/07/2025, Siku Kuu ya Mt. Maria Magdalena, Mfuasi wa Wafuasi.
3. Halmashauri ya parokia inatoa shukrani kwa akina mama pamoja na wakristu wengine wote kwa kufanikisha mchango wa wiki iliyopita. Tulichanga ifuatavyo;
Misa ya kwanza: shs. 40,020.00 Misa ya nne shs. 32,780.00
Misa ya pili: shs. 25,585.00 Misa ya tano shs. 980.00
Misa ya tatu shs. 38,300.00 Mpesa – paybill. shs. 21,796.00
Mauzo ya vitambaa shs. 27,700.00
Pesa taslimu zilizochangwa siku hiyo ni shs. 187,121.00
OLF Women deposit kwa account shs. 135,000.00
Jumla ya pesa zote zilizokusanywa ni shs. 322,121.00.
4. Jumapili ijayo tarehe 26/7/2026 kutakuwa na semina ya wanaume wote baada ya Misa ya kwanza katika ukumbi wa CMA. Sote tunakaribishwa kwa lishe ya kiroho.
5. Mseminari wetu Bw. Raphael Muthini atakuwa anahitimisha utume wake wa kuwa pamoja nasi na atakuwa anarudi masomoni. Hivyo basi jumapili ijayo tarehe 26/7/2026 tunaombwa kumtolea shukrani vizuri.
Tangazo la Ndoa;
Kwa mara ya kwanza: Festus Mutia Mutinda, mwana wa Mutinda Kavii na Mukeli Mbai kutoka Kitui-Mbitini Kisasi, anakusudia kufunga ndoa na Sabina Elizabeth mwana wa Elizabeth Mbata kutoka Kitui-Mbitini Katwala.
Yeyote mwenye kizuizi cha ndoa hii amjulishe Baba Paroko



